Wawakilishiwa Afrika 
waliokuwa wamebakia katika michuano ya soka ya Olimpiki inayoendelea 
jijini London, Uingereza timu za Misri na Senegal zimetolewa katika 
hatua robo fainali ya michuano hiyo. Misri
 waliyaaga mashindano hayo baada ya kukubali kipigo cha mabao 3-0 kutoka
 kwa Japan wakati Senegal wenyewe walifungwa na Mexico mabao 4-2. Kwa
 matokeo hayo Japan watakutana na Mexico katika hatua 
ya nusu fainali 
wakati timu ambayo inapewa nafasi kubwa ya kunyakuwa medali ya dhahabu 
kwa mara ya kwanza katika michuano hiyo timu ya Brazil watakutana na 
Korea Kusini baada ya kufanikiwa kuifunga Honduras katika hatua ya robo 
fainali. Korea 
Kusini walitinga katika hatua hiyo baada ya kufanikiwa kuwaondosha 
wenyeji Uingereza kwa changamoto ya mikwaju ya penati baada ya timu hizo
 kwenda sare ya bao 1-1 katika dakika 120 walizocheza. Nusu
 fainali ya michuano hiyo inatarajiwa kufanyika Jumanne ambapo Brazil na
 Korea Kusini watakutana katika Uwanja wa Old Traford uliopo jijini 
Manchester wakati Mexico na Japan wenyewe watacheza katika Uwanja wa 
Wembley jijini London.  
 
 
No comments:
Post a Comment