 
 
Kiungo wa kimataifa wa 
Ufaransa, Samir Nasri huenda akafungiwa kucheza michezo ya kimataifa kwa
 miaka miwili baada ya kumshambulia mwandishi wa habari katika michuano 
ya Ulaya mwaka huu. Kiungo huyo alikwaruzana na mwandishi wa Ufaransa 
baada ya timu hiyo kung’olewa 
    katika robo fainali ya michuano ya Ulaya 
baada ya kukubali kipigo cha mabao 2-0 kutoka kwa Hispania. 
Nasri ambaye
 aliingia katika mchezo huo kama mchezaji wa akiba alimjibu mwandishi 
huyo kwa lugha chafu baada ya kuulizwa swali kuhusiana na mchezo huo 
mara baada ya kumalizika. Hiyo inakuwa ni mara ya pili kwa mchezaji huyo
 kuingia katika mzozano na mwandishi huyo ambapo mara kwanza 
alishangilia bao akimwambia mwandishi huyo kufunga mdogo wake wakati 
alipofunga bao ya kusawazisha dhidi ya Uingereza katika mchezo wa 
ufunguzi wa kundi D dhidi ya Uingereza. Rais wa Shirikisho la Soka la 
Ufaransa-FFF, Noel le Graet amesema kuwa tukio alilofanya mchezaji huyo 
halivumiliki na kumuonya Nasri kuwa anapaswa kuzuia hasira zake katika 
siku mbeleni. 
 
 
No comments:
Post a Comment