
Wachezaji wa soka wa timu
 ya taifa ya Korea Kusini wameongezewa motisha ya kutolitumikia jeshi la
 nchi hiyo kama watafanikiwa kuwafunga wapinzani wao Japan na kunyakuwa 
medali ya shaba katika michuano ya olimpiki. Hatua
 hiyo ni ya kushangaza toka mshambuliaji wa kimataifa wa nchi hiyo 
anayecheza klabu ya Arsenal Park Chu-Young kuachwa katika kikosi cha 
timu hiyo katika mechi za kufuzu michuano ya Kombe la Dunia na 
kulazimika kuomba msamaha kwa kuchelewa kujiunga na jeshi na kuchukua 
uraia wa Monaco. 
Akihojiwa
 kuhusiana na suala hilo, Kocha wa timu hiyo Hong Myung-Bo alikiri kuwa 
ni kweli kama wakipata medali ya shaba ya kushika nafasi ya tatu katika 
michuano hiyo wachezaji watapata msamaha wa kwenda jeshini kitu ambacho 
ni lazima kwa raia yoyote kwa Korea Kusini. Kocha
 huyo aliendelea kusema kuwa suala hilo halina umuhimu sana kwani 
madhumuni yao makubwa ni kuifunga Japan na kuwapa furaha mamilioni ya 
mashabiki watakaokuwa wkiwatizama huko nyumbani. Japan
 imewahi kutwaa medali ya shaba katika michuano ya olimpiki iliyofanyika
 jijini Mexico City mwaka 1968 na wamepata nafasi hiyo tena dhidi ya 
mahasimu wao Korea Kusini baadae leo mchezo ambao unatarajiwa kuwa mkali
 na kusisimua.  
 
 
No comments:
Post a Comment