
Yen Shuwen. 
Muogeleaji kinda kutoka 
China Yen Shiwen ameshinda medali yake ya pili ya dhahabu ya mita 200 
katika michuano ya kuogelea ya Olimpiki inayoendelea jijini London. 
Shiwen mwenye umri wa miaka 16 ambaye alishinda medali ya dhahabu pia 
katika mashindano hayo ya mita 400 kwa kutumia muda wa dakika 7.57 na 
kuweka rekodi ya muda wa kasi zaidi katika michuano hiyo. Katika 
mashindano hayo Alicia Coutts alishika nafasi ya pili na kupewa medali 
ya fedha akitumia muda wa dakika 2.08.15 wakati Caitlin Leverenz wa 
Marekani alishinka nafasi ya tatu na kupata medali ya shaba akitumia 
muda wa dakika 2.08.95. Katika michuano hiyo China inaongoza kwa 
kunyakuwa medali nyingi zaidi ikiwa imejikusanyia medali 23, dhahabu 13 
fedha sita na shaba nne, nchi inayofuatia ni Marekani nayo ikiwa na 
idadi sawa ya medali 23 lakini wenyewe wakiwa na dhahabu tisa fedha nane
 na shaba sita. Nchi ya tatu kwa wingi wa medali mpaka sasa ni Ufaransa 
ambayo imenyakuwa medali 11, medali nne za dhahabu, tatu za fedha na nne
 za shaba.
 
 
No comments:
Post a Comment