
 Jack Wilshere.
Meneja wa klabu ya 
Arsenal Arsenal Wenger amesema kuwa kiungo nyota wa klabu hiyo Jack 
Wilshere hata kuwa sehemu ya kikosi chake katika michezo ya mwanzo wa 
Ligi Kuu nchini Uingereza kutokana na majeraha yanamsumbua. Wilshere
 ambaye ana miaka 20 alishindwa kucheza msimu uliopita kutokana na 
kufanyiwa upasuaji wa goti aliofanyiwa Mei mwaka jana. Wenger
 ambaye alikuwa akizungumza na waandishi wa habari kabla ya kukamilisha 
ziara ya bara la Asia jijini Hong Kong amesema kuwa anatarajia mchezaji 
huyo kurejea dimbani mwezi Octoba. Wakati
 akiuguza goti lake Wilshere alilitonesha tena wakati akifanya mazoezi 
ili arejee uwanjani na hivyo kumfanya mchezaji kukosa michuano ya Ulaya 
iliyomalizika Julai mosi mwaka huu ambapo anatarajiwa kuanza mazoezi 
mepesi Agosti na akitarajia kurejea uwanjani Octoba.   
 
No comments:
Post a Comment