Tuesday, July 31, 2012

TASWIRA MBALIMBALI ZA WANAFUNZI WA SHULE MBALIMBALI MUDA MFUPI BAADA YA MGOMO WA WALIMU KUANZA NCHINI.

Wanafunzi wa shule za msingi Vwawa wakiwa wanapiga vidumu huku wakielekea ofisi ya mkuu wa wilaya ni Baada ya walimu kugoma.
 
Wanafunzi wakiwa wanaelekea ofisi ya Mkuu wa wilaya.
 
Wanafanzi wa darasa la saba shule ya msingi Meta wakiendelea kupeana mazoezi ya masomo mbalimbali baada ya waalimu wao kugoma kuingia madarasani
 
Moja ya wanafunzi wa shule ya msingi Meta baada ya kuona walimu hawajaingia darasani yeye alichukua jukumu la kuwafudnisha wenzake
 
Wanafuzi wapo makini kumsikiliza mwanafunzi mwenzao.
 
Baadhi ya wanafunzi wa darasa la saba shule ya msingi Makuburi, wakijisomea baada ya walimu shuleni hapo kugoma kufundisha jana Julai 30, 2012. Mwalimu Mkuu wa shule hiyo, ambaye hata hivyo alikataa kutaja jina lake, alisema walimu walifika lakini hawakufanya kazi wakiunga mkono agizo la rais wa chama cha walimu Gratian Mukoba, aliyewataka walimu wote kushiriki mgomo usio na kikomo kuanzai leo Jumatatu.
 
Kiongozi wa wanafunzi walioandamana jana jijini Dar es Salaam, Christofa Msifuni Msuya wa darasa la saba, shule ya msingi Bwawani, akizungumza kwa niaba ya wenzake kwenye ofisi za Afisa Elimu wa Manispaa ya Temeke jijini Dar es Salaam Jumatatu Julai 30, 2012.
 
Afisa Elimu Taaluma wa Manispaa ya Temeke jijini Dar es Salaam, Juliana Mlay (Kushoto) akitafakari nini cha kuwaambia "Wageni" wake, wanafunzi wa shule za msingi Kijichi na Bwawani za jijini walioandamana umbali wa kilomita 10 hadi ofisini hapo wakilaani kutosoma jana, kufuatia mgomo wa walimu ulioanza nchi nzima jana Julai 30, 2012.
 
 
Wanafunzi wa shule za msingi Bwawani na Kijichi, zajijini Dar es Salaam, wakiamnadmana jana kupinga kile walichokiita kuvurfughwa kwa haki ya mtoto ya kupata elimu, na hii ni kufuatia mgomno wa walimu ulioanza jana nchi nzima. Wanafunzi hao waliandamana hadi urefu wa kilomita 10 kutoka shuleni kwao hadi ofisi ya Afisa Elimu wa Manispaa ya Temeke, ziliko shule hizo, jirani na uwanja wa taifa ili kufikisha kilio chao.
 
 
Mwanafunzi wa darasa la kwanza shule ya msingi muungano akiwa nje ya shule akichezea mchanga maana walimu wamegoma
 
Wanafunzi wa shule za Makuburi na Mabibo, wakiwa chini ya mwembe, jana asubuhi Jumatatu Julai 30. Walimu wengi hawakuingia madarasani kufundisha jana wakiitikia mwitoi kutoka chama cha walkimu nchini kilichowataka kutofanya kazi jana Jumatatu na kuendelea hadi madai yao kuhusu maslahi yatakaposhughulikiwa na serikali.
 
Wanafunzi wa shule ya msingi Ipembe, Nyerere, Unyankindi na Singidani katika Manispaa Singida.Picha Zote na Mdau Nathaniel Limu,Khalfan Hamis na Wadau wa Mbeya Yetu

No comments: