Tuesday, July 31, 2012

HARUFU YA RUSHWA YA PENYA NDANI YA BUNGE LA TANZANIA.

Kufuatia kuwepo kwa malalamiko ya vitendo vya Rushwa kuugubika  ndani Muhimili wa Bunge Tanzania na kusababisha kuvunjwa kwa kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini mwishoni mwa wiki iliyopita,
baadhi ya wabunge wametaka majina ya wenzao wanaojihusisha na Rushwa yawekwe wazi na wafukuzwe bungeni.
Akichangia hoja mara baada ya kumalizika kwa kipindi cha maswali na majibu, Mbunge wa Arumeru Mashariki Joshua Nassari amesema licha ya kamati ya Nishati na madini kutajwa moja kwa moja pia zipo kamati nyingine ambazo wabunge wake wanatajwa kuhusika na vitendo vya kuomba rushwa.
Kwa upande wao Mbunge wa Lindi Mjini Salum Khalfan na Mbunge wa Nkasi Kaskazini Ally Keissy Mohamed wamelitaka bunge kuwafukuza bungeni wabunge watakaobainika kujihusisha na vitendo vya rushwa.
Baada ya kutolewa kwa hoja hizo, Naibu Spika wa Bunge JobNdugai ameagiza Kamati ya Uongozi wa Bunge kukutana na Spika Anne Makinda ili kulipatia ufumbuzi suala hilo ambalo ni zito ndani ya chombo hicho cha kutunga sheria.
Mbali na suala hilo ambalo limetikiza Bunge pia hii leo Waziri wa Afya na Uatawi wa Jamii Dk Hussein Mwinyi amewasilisha  makadirio ya Bajeti ya wizara hiyo kwa mwaka wa fedha wa 2012/2013 ambapo moja ya vipaumbele vyake ni  kutatua tatizo la kuongezeka kwa vifo vya akinamama wajawazito na watoto wakati wa kujifungua.
Kambi rasmi ya Upinzani Bungeni nayo imepata fursa ya kuwasilisha Bajeti yake Kivuli ya mapato na matumizi ya Wizara ya Afya ambayo imesomwa na mbunge wa Viti Maalum Chadema, Conchester Lwamlaza.

No comments: