Tuesday, July 31, 2012

VIDEO YA NEY NUSURA IMTOE ROHO.

 
Staa wa muziki wa  kizazi kipya Bongo,  anayemiliki jina la Ney wa  Mitego amenusurika  'kudanja' kufuatia  mlipuko mkubwa wa moto wakati alipokuwa  akikamilisha zoezi la upigwaji picha (shooting) za video za wimbo wake mpya uliopewa jina la  Nasema nao ambao ndani ametoa diss kibao kwa  wasanii kadhaa wa muziki huo. Akizungumza na media muda mfupi uliopita  Ney ambaye sasa amejipachika jina  la 'True Boy'
amesema kuwa kulikuwa na matukio mengi ya kushangaza wakati  kuanza kwa zoezi la kuchukua video hiyo ikiwemo watu kuungua moto na  wengine kukatwa na mabati wakati  wa harakati hizo


 "Wakati tunaanza tu kuna mdogo wangu alikatwa na bati, halafu baada ya muda  tulishangaa mapipa yaliyokuwepo hapo yanalipuka moto mkubwa na  kumuunguza vibaya 'dairekta' wangu huku mimi nikinusurika  baada ya  kuruka na kutua upande wa pili, mwanzoni hatukujua kama jamaa ameumia sana lakini baada ya  kumcheki siku iiyofuata tuligundua kuwa amebabuka vibaya na ngoozi yote ya mkono imetoka kabisa"  alisema  Ney

No comments: