Tuesday, June 19, 2012

UPEPO WA AFRIKA MASHARIKI KUINGIA KWENYE ANGA ZA D’BANJ NA P SQUARE.


Naona 2012 Afrika inazidi kushika, ni mwaka ambao tumewaona vijana wa kiafrika wakifly high kwenye muziki wa dunia, alianza Mnigeria D’banj na kutoa single ya Oliver Twist akiwa chini ya lebo ya Good Music ya Kanye West na baadae kidogo wanigeria P SQUARE nao wakatoa kolabo
na Akon, hakija kaa sawa P Square wakaongoza mfululizo kwenye habari za burudani Afrika baada ya kuachia kolabo yao na Rick Ross.

Alpha akiwa na wazazi wa mastaa waimbaji Ray J na Brandy.

Upepo nauona kama unahamia Afrika Mashariki anytime soon, Ay ameshatangaza kolabo zale na Young Joc, Tyga na Tanto Metro and Devonte wa Jamaica, jipya lililonifanya nikupe hiyo intro, ni kuhusu mshkaji Mrwanda ambae wiki kadhaa zilizopita aliweka picha kwenye facebook akiwa kwenye party na mastaa wa dunia kama  Ray J, baba yake Nick Cannon mume wa Maria Carey na mkali wa reggae Lady Dread.
Hizo line zinamuhusu Mwimbaji ambae ni mshindi mara mbili wa shindano la Tusker Project fame Alpha Rwirangira wa Rwanda ambae yuko Marekani sasa hivi akipiga kitabu cha muziki, amethibitisha kwamba single yake mpya inayokuja iitwayo I SWEAR imetengenezwa na mikono ya producer wa Hollywood Marekani KENNY CLOUDS ndani ya jumba la studio ya BLACK HOLE PRODUCTION.
Kinachotoa imani zaidi ya ukali wa hiyo single ni kwamba Huyo Producer nimekutajia tu lakini naona jina limekupita, lakini ni maarufu na mikono yake sasa hivi ndio inahusika kufanya mixing ya album mpya ya Snoop Dogg huyu huyu unaemsikia na kumuona.

No comments: