Ulishajiuliza kwanini Diamond yuko smart sana kwa namna anavyozipeleka issue zake za muziki? Hushangai iweje msaniii huyu ambaye wengi walitegemea awe na elimu ya chuo kikuu ndio aweze kuufanya muziki kwa umaridadi mkubwa kiasi cha kutochuja kwa show zake japo zinajipanga kama mayai kwenye tray!
Well, wengi hili wanaweza kuwa wanalijua juu juu tu ama hawalijui kabisa kuwa the person behind Diamond’s music creativity is none other than Ruge Mutahaba!!
Yeah, habari ndio hiyo, hate it or love it.
Tangu show ya aina yake ya Diamonds Are Forever iliyowapa mkwanja mnene wa kuweka benki na kula bata, show ya Dar Live iliyompa sifa Diamond kwa kutua kwenye ‘Uwanja huo wa taifa wa burudani mpaka show ya Big Brother Stargame aliyoifanya mwaka huu. He (Ruge) was the mastermind!
- Diamond na washikaji.
Kuna mtu mmoja wa karibu sana na Diamond hivi karibuni ametuambia kuwa maandalizi ya show ya ‘Diamonds Are Forever ya pale Mlimani City yalichukua takribani wiki nzima. Ruge alikuwa akienda kila siku kuangalia maendeleo ya rehearsal and he was like, “mmh mmh! Hapo bado,ongezeni nguvu zaidi.”
Kwenye show ya hivi karibuni ya Miss Redds Tanzania huko Arusha, Ruge alionekana kwenye picha akimwelekeza Diamond namna ya kupiga kinanda na ngoma. Haijalishi kama anajua kupiga hivyo vitu ama la,hilo si suala letu, cha msingi ni kuwa ushauri wake unafanya kazi kwa Diamond.
- Ruge akimpa maelekezo Diamond kuhusu Drums.
- Ruge akimpa somo la kinanda Diamond.
No comments:
Post a Comment