Tuesday, June 19, 2012

HII NDIO HELIKOPTA NYINGINE YA KENYA ILIYONUSURIKA KWENYE AJALI




Ikiwa ni wiki moja tu imepita toka kutokea ajali ya Helikopta huko Kenya iliyochukua maisha ya watu sita wakiwemo mawaziri wawili, asubuhi ya June 18 2012 wasiwasi ulienea tena  kwenye mji wa Karatina huko Kenya baada ya HELIKOPTA kutua ghafla shambani kutokana na hali mbaya ya hewa kwenye anga.

Standard Media wamesema mwandishi wao wa eneo la mlima Kenya amesema hiyo helikopta ni ya raia wa kigeni aitwae Allan Root  aliekua akiwapeleka watoto wake shule Nairobi.
Root anaishi kwenye eneo la Mbuga ya LEWA na alipofika eneo la Karatina alilazimika kutua kwa ghafla katika shamba moja eneo la Mathaithi karibu na Karatina kutokana na hiyo hali mbaya ya anga ambayo kama angeendelea kusafiri kulikua na uwezekano mkubwa wa ajali kutokea.

No comments: