Wednesday, June 27, 2012

MANJI AWEKEWA PINGAMIZI TFF ASIGOMBEE YANGA.

Manji kulia, akiwa amechuchumamaa kumsalimu Bi Rukia, mwanachama maarufu wa Yanga.
Wakati kamati ya uchaguzi ya Shirikisho la soka Tanzania (TFF) inatarajiwa kuketi Julai 2 kwa ajili ya kupitia pingamizi zilizowasilishwa kwa wagombea uongozi wa klabu ya Yanga, wagombea wawili Yusuf  Manji na Stanley Yono Kevela wamewekewa pingamizi. 
Klabu ya Yanga inatarajiwa kufanya uchaguzi mdogo julai 15 jijini Dar es Salaam ili kuziba nafasi za baadhi ya viongozi waliojiuzulu akiwemo mwenyekiti Lloyd Nchunga.
 Mjumbe wa kamati hiyo iliyo chini ya mwenyekiti wake Deogratius Lyatto, Salum Mbwezeleni alisema kwamba kamati yake itapitia pingamizi hizo kwa kusikiliza wapingaji na waliopingwa na kisha kutoa maamuzi.
Hata hivyo, Mbwezeleni hakuweza kutoa ufafanuzi wa pingamizi wa wagombea hao Manji (Uenyekiti) na Kevela (Makamu Mwenyekiti, Ujumbe) kwa madai kuwa bado hajapitia maelezo yaliyowasilishwa na waliopinga.
 “Ninachoweza kusema kwa sasa ni kuwa kamati itakutana Julai 2 na kuwasikiliza wahusika wote na kisha tutatoa maamuzi ili majina yaweze kutangazwa na wagombea waanze kampeni zao,”alisema. 
Kamati ya uchaguzi ya Yanga chini ya mwenyekiti wake Jaji Mstaafu John Mkwawa wiki iliyopita ilitawataja waliopitishwa katika ujumbe ni pamoja na Jumanne Mwamenywa,Edgar Fongo, Beda Tindwa, Ramadhan Said,Omary A. Ndula, Shaban Katwila,Ramadhan Y. Kampira,Lameck Nyambaya na Peter H. Haule. 
Wengine ni  Justine S. Baruti,Abdalah A. Mbaraka, Kevela,Mosess K. Valentino,Aaron Nyanda,George M. Manyama.Abdalah Sharia Ameir,Jamal Kisongo na Gaudiusus Ishengoma. 
Huku wanaowania nafasi ya Makamu Mwenyekiti ni Ayoub Nyenze, Kevela na Clement A. Sanga, wakati Jonh Paul Jambele, Manji, Edgar W. Chibula na Sarah Ramadhan wameomba katika nafasi ya uenyekiti,”alisema. 
Uchaguzi huo ambao umepangwa kufanyika Julai 15 mwaka huu, umelenga kuziba nafasi ya Mwenyekiti, Makamu Mwenyekiti na wajumbe wanne wa kamati ya Utendaji ambao walijiunzulu.
 

No comments: