- Prezzo akishukuru kabla ya kuondoka uwanja wa ndege.
Mwakilishi wa Kenya katika shoo ya Big brother StarGame 2012, msanii Prezzo amewasili jijini Nairobi (Kenya) jana asubuhi na kufuta minong’ono iliyokuwa imezagaa nchini humo kuwa ana bifu na aliyekuwa mshiriki mwenzake katika shindano hilo Alex Malonza.
Akiongea baada ya kuwasili jijini Nairobi jana Prezzo alisema hadhani kama ana kinyongo na aliyekuwa mshiriki mwenzake. Tunamnukuu “I held no grudges with Malonza, even though he nominated me twice”. Akimaanisha hana kinyongo na Malonza ingawaje alimpigia kura ya kutaka awe mmoja wa wanaotakiwa kutoka mara mbili.
Akiendelea prezzo alisema nimesikia anataka kufanya kazi za kisanii na mimi, sidhani kama nina tatizo na hilo kwani sina kinyongo nae. Mimi nipo kwa ajili ya chochote ambacho kitafanya mkono uende kinywani kwa hivyo tusubiri na kuona matokeo ya kile kinachofikirika ama kitakachowezekana.
akijibu swali la kama bado anampenda mshiriki mwenzake toka Nigeria Prezzo alijibu tumeongea na tutakutana Nairobi siku si nyingi nafikiri bado kuna nafasi ya kujadiliana kwa mapana zaidi.
Prezzo ameshika nafasi ya pili katika shindano la mwaka huu na kupata nafasi ya kuteuliwa kuwa balozi wa kampeni ya kupiga vita njaa “One Campaign” na pia amepata nafasi ya kwenda nchini Marekani baadae mwishoni mwa mwezi huu kushuhudia shoo ya rapa nguli wa hip hop Jay Z jijini New York.
Kuwasili kwa prezzo jana asubuhi katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Jomo Kenyatta kulipelekea shughuli kusimama katika uwanja huo kwani watu wengi waliacha shughuli zao na kwenda kumlaki huku wakimpongeza kwa kufika hatua ya fainali na kukosa ushindi kidogo na wengine wakimpa mkono pamoja na kumkumbatia na kupiga naye picha. Prezzo anatarajiwa kukutana na Makamu wa Rais wa Kenya Mheshimiwa Kalonzo Musyoka muda wowote leo au kesho
- Prezzo akitoa ishara ya pamoja.
- Prezzo akiwa na mama yake ndani ya gari lililompeleka nyumbani.
- Prezzo akihojiwa.
- Prezzo akipozi na fan wake.
- Prezzo akisalimiwa.
No comments:
Post a Comment