
Mkurugenzi wa Takwimu za Uchumi wa 
Ofisi ya Taifa ya Takwimu Bw. Morrice Oyuke akiongea na waandishi wa 
habari leo jijini  Dar es Salaam kuelezea hali ya Ukuaji wa Pato la 
Taifa kwa 7.1% katika  kipindi cha robo mwaka 2012.
Ofisi ya Taifa ya 
Takwimu (NBS) imetoa taarifa ya hali ya uchumi nchini na kufafanua kuwa 
 pato la taifa  la Tanzania limekua kwa  asilimia 7.1 katika kipindi cha
 robo ya mwaka 2012  ikilinganishwa  na asilimia 6.1  za mwaka jana.
Ukuaji huo wa asilimia
 7.1 unatokana na ongezeko la uzalishaji katika shughuli mbalimbali za 
kiuchumi zikiwemo za kilimo, Uvuvi, Viwanda, Ujenzi na  zile za utoaji 
wa huduma mbalimbali za jamii.
Akitoa taarifa hiyo 
jana jijini Dar es salaam Mkurugenzi wa Takwimu za Uchumi  wa Ofisi ya 
Taifa ya Takwimu Bw. Morrice Oyuke amesema kuwa lengo la  utoaji wa 
taarifa hizo kwa vipindi vifupi vya vya  robo mwaka unalenga kuwapatia 
wadau wa Takwimu za Pato la Taifa uwezo wa kutathmini mabadiliko ya 
ukuaji wa uchumi nchini.  
Amesema kuwa jumla ya 
thamani ya pato la Taifa katika kipindi cha robo ya mwaka 2012 ni 
shilingi 4,220,535 milioni ikilinganishwa na kiasi cha shilingi milioni 
3,940,261 za mwaka 2011.
Amefafanua kuwa ukuaji
 wa shughuli uzalishaji katika shughuli za kilimo nchini  ulifikia 
asilimia 1.4 katika kipindi cha robo ya kwanza ya mwaka 2012  
zikilinganishwa na asilimia 1.2 katika kipindi hicho kwa mwaka 2011  
kutokana na upatikanaji wa mvua za kutosha nchini katika mikoa  
inayozalisha mazao kwa wingi. 
 Amesema ukuaji katika
 shughuli za uvuvi ulikua  asilimia 2.6 katika robo ya kwanza ya mwaka 
2012 huku shughuli za uchumi katika  sekta ya viwanda na Ujenzi ambayo 
inahusisha uchimbaji wa madini na  kokoto ikikua kwa asilimia 14.3 
ikilinganishwa na 0.8% za mwaka 2011.
Bw. Oyuke ameongeza 
kuwa ongezeko hilo  la uzalishaji wa madini ya dhahabu linatokana na 
uzalishaji wa wa madini  ya dhahabu kutoka kilo 8,140 kwa mwaka 2011 
hadi kufikia kilo 16,736 kwa mwaka 2012.
Pia amebainisha kuwa  
shughuli za utoaji wa huduma za biashara za jumla na  rejareja, 
ukarabati wa magari na pikipiki na vifaa vingine vya majumbani katika 
kipindi hicho zilifikia asilimia 9.0 huku shughuli za  upangishaji 
nyumba na biashara zikiwa 8.2 %, uchukuzi na mawasiliano  16.4%, hoteli 
na migahawa 3.8%, Benki asilimia 15 shughuli za uendeshaji  serikali 
6.4%, Elimu 6.1% na utoaji wa huduma za Afya nchini zikikua kwa kasi ya 
asilimia 5.1.
 
 
No comments:
Post a Comment