Tuesday, July 31, 2012

AIRTEL WAENDELEA KUBORESHA AIRTEL MONEY.


Meneja Uhusiano wa Airtel Tanzania, Jackson Mmbando akizungumza na Waandishi wa Habari, wakati wa uzinduzi wa namba fupi *150*60# itakayotumika kupata orodha
(Menu) ya Airtel Money pamoja na kuzindua promosheni inayomuwezesha mteja wa Airtel kutuma na kupokea pesa bure. Kulia ni Afisa Uhusiano wa Airtel Tanzania, Jane Matinde. Uzinduzi wa promosheni na utambulisho wa namba hiyo fupi ulifanyika katika makao makuu ya Airtel mjini Dar es Salaam jana.

Kampuni ya simu za mkononi ya Airtel Tanzania, imeendelea kuboresha huduma ya Airtel Money kwa kurahisisha upatikanaji wa mwongozo (menu) kwa kupiga **150*60# Bure, pamoja na kuzindua promosheni kabambe itakayowawezesha wateja wa Airtel nchi nzima kutuma pesa bure.
Akizungumza wakati wa uzinduzi wa huduma hiyo, Meneja Uhusiano wa Airtel Tanzania, Jackson Mmbando alisema;” “Airtel tunaendelea kutoa uhuru kwa wateja kupata
huduma zetu, kwa urahisi zaidi nchini kote, kuanzia sasa mteja akipiga **150*60#, anapelekwa moja kwa moja kwenye orodha yake ya huduma na kuweza kuchagua
anachohitaji kufanya, ikiwa ni pamoja na kuongeza salio, kufanya malipo,
kutoa pesa na mengine mengi, alisema: “Tumefanya hivi, ili kumwezesha mteja mwenye simu yeyote kupata huduma za
kibenki na kuondoa changamoto zozote zitakazojitokeza, sasa mteja ana uhuru wa kuchagua kutumia njia ya awali, ambayo ni kwenda moja kwa moja kwenye mwongozo wa simu yake na kupata orodha (Menu) ya Airtel au kupiga namba *150*60# na kuunganishwa moja kwa moja,”alisema.
“Vile vile tunayo furaha kuzindua ofa kabambe kwa wateja wetu nchini zima, ambapo kutuma au kupokea pesa chini ya kiwango cha 100, 000 ni BURE na mteja atakaponunua LUKU kupitia Airtel Money ni BURE (hakuna viwango vya miamala vitakavyotozwa). 
Tunawajulisha wateja wetu wote na wakala wetu waliosambaa nchi zima kutumia huduma hii iliyo rahisi ni rahisi,” aliongeza Mmbando.
Airtel Tanzania ni mtandao ulioenea nchini na unatoa huduma za kifedha za Airtel Money yenye mawakala zaidi ya 10,000 waliosambaa maeneo mbalimbali mjini na vijijini kwa dhamira ya kupunguza changamoto ya upatikanaji wa huduma za kifedha na kusaidia wateja wetu kuokoa muda kwenda mbali kupata huduma za kibenki.
Kupitia Airtel Money, mteja anaweza kupata huduma mbalimbali ikiwemo: kupokea pesa, kulipa bill kama DSTV, LUKU na DAWASCO, USA visa , kununua salio na huduma nyingine nyingi.

No comments: