Wednesday, June 20, 2012

" WATANITEKA WAKIWA RUMANDE " BAGHDAD

Bwa’ mdogo anayekuja juu kwa kasi kwenye anga ya muziki wa kizazi kipya Bongo, Christopher Kweka ‘Baghdad’ aliyetangaziwa hatari na baadhi ya wasanii wanaong’arisha nyota zao kupitia muziki huo amesema watafanikiwa zoezi hilo wakiwa rumande.

 
Akizungumza muda mfupi uliopita Baghdad amefunguka kuwa ameshangazwa na hatua za wasanii hao kuchukia na kuamua kumtishia maisha kufuatia 'interview' yake na Gossip Cop wa XXL huku wakijua kuwa
alichokisema kilikuwa ni ukweli kwa lengo lengo la kuwafungua watu kuhusiana na matatizo wanayokumbana nayo wasanii wanapokuwa kwenye kazi zao
“Labda wataniteka wakiwa rumande, kwani nimeshalifikisha suala hili polisi na tayari wamepewa saa 48 kuripoti” kituoni alisema Baghdad.
Baghdad kilinuka upande wake kufuatia stori iliyovujisha kwenye interview hiyo kuwa wasanii Mabeste, Suma Mnazareti,Tash na Mensen Selecta walilala mchongoma (chumba kimoja) kufuatia promota aliyewapeleka pande hizo kusepa bila kuwapa mkwanja waliokuwa wamekubariana na hali kuwa mbaya upande wao.

No comments: