Tuesday, June 26, 2012

NGORIKA LAPATA AJALI.



Basi la kampuni ya Ngorika limepata ajari jana 25/6/2012 majira ya asubuhi pale maeneo ya kwa mrefu Mkoani Arusha wakati likianza safari kuja dar es salaam likiwa na abiria 54. Ajali hiyo imetokea wakati dereva akiwa kwenye mwendo wa kawaida tu ambapo ghafla kwenye eneo wanapopaita kibao cha njano kabla ya mteremko wa daraja la Nduluma dereva alishangaa kuona gari jingine likiwa limetokea mbele yake bila ya kujua limetokea wapi na alipojaribu kulikwepa
ndipo basi lilipopoteza welekeo na kupinduka, Lakini hakuna abiria aliyeripotiwa kufariki bali abiria wengi walilipotiwa kujeruhiwa kwenye ajali hiyo.

No comments: