
Kamanda Kova .
Kamanda wa polisi Kanda Maalum ya Dar es salaam Kamanda Suleiman Kova
akizungumza na waandishi wa habari kuhusu tukio la utekaji nyara na
kujeruhi lililompata kiongozi mgomo wa Madaktari Steven Ulimboka
anayedaiwa kutekwa na watu watano wakati akipata kinywaji katika klabu
ya Leaders Kiondoni jijini Dar es salaam.

Waandishi wa habari waimsikilza kamanda Suleiman Kova katika kituo kikuu cha polisi Kati jijini Dar es salaam leo mchana.
Kamanda Kova amesema Ulimboka aliokotwa na msamaria mwema ambaye
hakutaka kumtaja jina lake kiusalama na kutoharibu upelelezo kuwa
msamaria mwema huyo alimuokota Ulimboka katika msitu wa Mabwepande na
kutoa taarifa kituo cha polisi cha Bunju, ambapo polisi aliyekuwa zamu
alichukua maelezo yake na baadae Steven Ulimboka kuletwa katika
hospitali ya taifa ya Muhimbili kwa matibabu zaidi.
Dk Steven
Ulimboka akiwa amejruhiwa vibaya na watu wasiojulikana baada ya kutekwa
na kupigwa vibaya usiku wa kuamkia leo na kuokotwa huko Mabwepande.
Kamanda Kova amesema jeshi la Polisi Kanda Maalum limeunda jopo maalum
kwa ajili ya uchunguzi na upelelezi wa tukio hilo la utekaji nyara,
kwani ni tukio la kwanza kutoke nchini, ameongeza kwamba wahusika wote
watakaobainika kuhusika na tukio hilo wachukuliwa hatua za kisheria na
sheria itafuata mkondo wake ili kukomesha matukio mengine kama hayo.
No comments:
Post a Comment