Friday, June 22, 2012

KOFII NA MKEWE ALIYAH WALIPOONYESHA JUMBA LAO LA KIFAHARI

Mwanamuziki Koffi Olomide alitambulisha jumba lake kwenye sherehe ya ufunguzi wa jumba hilo ambalo limegharimu mamilioni ya shilingi na kunakshiwa kwa samani za bei ghali.
Mashabiki walipokea kwa hisia tofauti kitendo cha Mwanamuziki Koffi Olomide kuweka wazi Jumba lake la
kifahari huku wengine wakimpongeza na wengine wakimwambia kitendo hicho ni kama dhihaka kwa wacongoman ambao wengi wao wanaishi kwenye dhiki kali huku weingine wakiwa wanataabika kupata mlo wao lakini wanajitolea kuchanga kununua kazi zake au kuingia kwa show zake.
Kiukweli ni jumba la kifahari sana na alialika watu mashahuri kwenye sherehe hii ambayo ilitumia pesa nyingi.
Jumba hili limejengwa kwenye vilima vya Fleury almaarufu kama a mont-fleury eneo maarufu kama Msaki ambapo watu wenye pesa ndio wanaishi huko. Koffi ni mmoja wa wanamuziki wakubwa si tu kwa Congo bali Afrika nzima ambaye kiukweli amekuwa na mafanikio makubwa tangu aanze muziki na amejizolea mashabiki wengi kote Ulimwenguni kutokana na muziki wake.

No comments: