Friday, June 22, 2012

HATIMAYE NYAMWELA AAMUA KUMUOA DEMU ALIYEMPA MIMBA.



MWANAMUZIKI wa Bendi ya Extra Bongo ‘Wazee wa Kizigo Staili’, Hassan Musa ‘Super Nyamwela’ amevunja ukimya na kuamua kubeba jumla msichana alimpachika mimba aitwaye Hawa Maulid.
Super Nyamwela alifunga ndoa Jumapili iliyopita kwenye Msikiti wa Kinondoni-Studio, Dar es Salaam na
kufuatiwa na sherehe ‘hevi’ iliyofanyika nyumbani kwa Hawa maeneo hayo ya Kinondoni na kuhudhuriwa na watu mbalimbali wakiwemo mastaa wenzake.
Baada ya ndoa, jioni ya siku hiyo pati nyingine ya kukata na shoka iliendelea kwenye Ukumbi wa Meeda Sinza jijini Dar ambapo wageni waalikwa walipata nafasi ya kuserebuka huku wakila na kunywa na kuwatuza maharusi.

Super Nyamwela alisema anamshukuru Mungu kwa kumpatia mke mwema kwa mara nyingine baada ya kukaa muda mrefu kutokana na mke wa kwanza kufariki na kumuachia watoto wawili.













No comments: